Saturday 12 January 2013

Re: [wanabidii] MWANGOSI NA DR ULIMBOKA WAMUWEKA PABAYA JK

Very interesting,
kuna mambo hata mimi huwa yananiumiza kichwa sana. Hili la rada kama alivyohoji Isango. But tatizo lililopo ni kwa mamlaka katika kutokuwa wazi zaidi kisheria, maana ukihoji sana unaambiwa eti hata kule Uingereza hakuna mahali watu hao walipotajwa kuwa wanahusika kufanikisha ununuzi huo kwa njia ya rushwa. Hilo linahitaji mjadala mpana sana. Lakini hili la anayetuhumiwa kumjeruhi Ulimboka, mimi nadhani tuiachie mahakama maana naamini mwisho wa siku Dk. Ulikomboka atatakiwa mtambua na hapo ndipo tutajua mbivu na mbichi na kila kitu kitafahamika. Again suala la ufisadi wa hao uliowataja wote - ndo hapo tunaposema mamlaka hazitendi haki panaonekana, maana hao nao wangekuwa wamesafishwa, kubanwa au kuhukuhumiwa kwa tuhuma zinazowaandama na inaonekana hata wao wanaridhika kuitwa mafisadi maana hawachui hatua ili yuujue ukweli wa mambo

2013/1/12 Josephat Isango <joseisango@yahoo.com>
Yona, nakuheshimu. Niambie kwa sheria na taratibu zipi za nchi, suala la Joshua Mlundi raia wa Kenya kushikiliwa muda wote asionane na Ulimboka ili tujue kama ndiye alihusika kumtesa au la, Yona, ni taratibu zipi za nchi na sheria unazotusadikisha zipo zitawashughulikia walionunua Rada kwa bei kubwa, na chenji imerudi hawachukuliwi hatua, Ni wapi wamfisadi waliotajwa kama Balali, Mramba, Gray Mgonja, Lowassa, Chenge, Karamagi, Rostam watafikishwa mahakamani kama wezi wengine? Polisi wametuhumiwa kuiba milioni 150 tu leo wameshikiliwa Dar, lakini hawa waliokwapua mabilioni tupo nao tena wanatucheka mtaani, na humu ninapochangia kwako wanacheka. Askari aliyepiga Picha na Lema kesi imekamilika kifungo miaka minne ila yule aliyeenda kugombea UVCCM yupo kazini. Nchi hii hatukatai sheria zipo na tatibu zake, je zinafuatwa? Hao wanaharakati wa Tanzania si ndio wakileta malalamiko yanawekwa uvunguni, wakiandamana polisi wanatumwa kuwajeruhi, kuwatia ulemavu, vitisho kibao kila sehemu hadi wanakosa uhuru wa kutoka. Iwe wako sahihi au hawako sahihi kupeleka Marekani, ninaona wanatumia "try right and error method". Mwindaji anarusha rungu akitegemea kubahatisha.

--- On Sat, 1/12/13, Yona Maro <oldmoshi@gmail.com> wrote:

From: Yona Maro <oldmoshi@gmail.com>

Subject: Re: [wanabidii] MWANGOSI NA DR ULIMBOKA WAMUWEKA PABAYA JK
To: wanabidii@googlegroups.com
Date: Saturday, January 12, 2013, 6:39 AM

Hii nchi inaendeshwa kwa sheria na taratibu zake zilizopo - Haiendeshwi na Washington wala New York wala matamko yao .


2013/1/12 Mohamedi Mtoi <mouddymtoi@gmail.com>
Kwa nini mseme kuwa sio Dr Kafumu? Kwa nini mu-msemee mtu ambaye tayari kasha sema tena kwa kukitilia shaka kile alicho sema?!

Kauli hii ya Kafumu inasadifu kilicho ndani ya mioyo ya viongozi waliooko kwenye utawala unao anguka.

Asicho kiamini Kafumu ndio ambacho hakiamini Bosi wake kuwa mahakama imetendeka kazi yake kumvua ubunge! Matokeo yake Bosi naye ana ishangaa mahakama kumvua Kafumu ubunge kama Kafumu anavyo shangaa alio waita wana harakati wa magharibi.

Huu ni msiba.
Sent from my BlackBerry® smartphone on the Tigo Tanzania Network

Date: Sat, 12 Jan 2013 12:40:56 +0000
Subject: Re: [wanabidii] MWANGOSI NA DR ULIMBOKA WAMUWEKA PABAYA JK

Nadhani huyu siyo Dr. Peter Kafumu aliyegombea ubunge Igunga na kama ni yeye maadinko haya yanatupa picha ya mhusika! Katika karne hii baadhi ya wasomi kama ndugu yetu, mwenye PhD, bado tunaona mfumo wa chama kimoja ni sahihi! Very Interesting! Kweli bado tuna mwendo mrefu na inatia shaka kama tutafika
Idriss Mussa
Sent from my BlackBerry® smartphone from Orange Botswana

From: Dr Peter D Kafumu <kafumu@yahoo.com>
Date: Sat, 12 Jan 2013 03:40:44 -0800 (PST)
Subject: Re: [wanabidii] MWANGOSI NA DR ULIMBOKA WAMUWEKA PABAYA JK

Hivi wale vijana aaliokufa morogoro na kule singida mbona wao hawatambuliki kuwa ni wahanga wa siasa hizi chafu za kiamgharibi za vyama vingi?

--- On Sat, 1/12/13, Mohamedi Mtoi <mouddymtoi@gmail.com> wrote:

From: Mohamedi Mtoi <mouddymtoi@gmail.com>
Subject: [wanabidii] MWANGOSI NA DR ULIMBOKA WAMUWEKA PABAYA JK
To: wanabidii@googlegroups.com
Date: Saturday, January 12, 2013, 8:44 AM

KUUAWA kikatili kwa mwandishi wa habari wa Channel Ten, Daudi Mwangosi na tukio la kutekwa, kuteswa kwa kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Steven Ulimboka, limechukua sura mpya ambapo sasa limetinga katika Seneti ya Marekani, Tanzania Daima Jumamosi limeelezwa.

Taarifa kutoka Washington nchini Marekani zinasema Rais Jakaya Kikwete amelalamikiwa rasmi katika Seneti na wanaharakati na watetezi wa haki za binadamu nchini, na kwamba masuala hayo sasa yatafikishwa kwenye Shirika la Umoja wa Mataifa la Kutetea Haki za Binadamu (UNHRC) kwa hatua zaidi.

Mbali na mauaji ya Mwangosi na tukio la Dk. Ulimboka, Rais Kikwete pia amelalamikiwa kwa kufumbia macho matukio mengi ya kuteswa na kuuawa kwa raia pamoja na kufungiwa kwa gazeti la kila wiki la uchunguzi la MwanaHalisi, kutoroshwa wanyama hai kwa kupelekwa nje ya nchi na hatua ya polisi kutumia silaha za kivita kupambana na raia wasio na silaha wakiwemo wanafunzi wanaoandamana.

Ripoti hiyo ya wanaharakati na watetezi wa haki za binadamu yenye kurasa 27, inatuhumu utawala wa Rais Kikwete kwa kukandamiza demokrasia kwa kutumia polisi na vyombo vingine vya dola.

Watetezi hao wa haki za binadamu, wamedai kuwa baada ya kufanikiwa kuingiza masuala haya ya ukiukwaji wa haki za binadamu katika Seneti ya Marekani, sasa wanafanya kila liwezekanalo kuhakikisha suala hili linafikishwa Umoja wa Mataifa kwa kile walichokiita, kuiadabisha serikali.

Kwa mujibu wa nyaraka zilizopatikana, na pia kusambazwa katika baadhi ya taasisi za habari, suala hilo liko mikononi mwa Seneta Kerry, ambaye baada ya majadiliano katika Seneti, ripoti hiyo itapelekwa UNHRC.

Habari zinasema baadhi ya wajumbe wa Seneti waliofanikiwa kuona ripoti hiyo wamemeshitushwa na kile walichokishuhudia katika picha zilizoambatanishwa.

Aidha, ripoti hiyo pia imeeleza jinsi rushwa ilivyoshamiri nchini, ukandamizaji juu ya uhuru wa maoni na matumizi mabaya ya vyombo vya dola kudhibiti vyama vya upinzani na kutumia silaha za kivita kupambana na raia wasio na silaha.

Ripoti hiyo ya kuishitaki Serikali ya Kikwete, pia imelaani vitendo vya polisi kusambaratisha maandamano ya wanafunzi wa shule za msingi jijini Dar es Salaam, walioandamana Julai 31, mwaka jana kupinga ukosefu wa walimu nchini.

Mgomo wa wanafunzi ulikuja baada ya walimu wa shule za msingi na sekondari kupitia jumuiya yao - Chama cha Walimu Tanzania (CWT) – kuitisha mgomo nchi nzima wa kutaka kuboreshwa kwa mazingira ya kazi zao, nyongeza ya mishahara na malimbikizo ya posho.

Nyaraka zilizowasilishwa na wanaharakati hao, zimeambatanishwa na picha zinazoonesha namna Jeshi la Polisi lilivyohusika kuuawa kwa Mwangosi, picha mbaya ya maiti ya mwanahabari huyo, na namna Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Iringa, Michael Kamhanda alivyokuwa akishuhudia askari wake wakimsulubu mwanahabari huyo kabla ya kufunga kazi kwa kumaliza uhai wake.

Kadhalika, kumeambatanishwa picha zinazoonesha maiti za watu waliouawa wakati wa maandamano huko Arusha, na ile inayosadikiwa kutokea kule Songea. Picha nyingine za kusikitisha ni zile zinazoonesha askari zaidi ya watano wakimdhibiti mwanaharakati mmoja katika maandamano, na umati wa wanafunzi wa shule za msingi wakiandamana, huku nyingine zikionesha askari mwenye silaha ya kivita akimsindikiza mwanafunzi wa kike mwenye mfuko wa madaftari.

Tangu mwaka 2005 ambapo masuala mazito ya rushwa yamekuwa yakiibuliwa, ikiwamo ununuzi wa rada feki, wizi wa fedha za umma kutoka kwenye Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), mkataba tata wa Richmond, ukusanyaji wa kodi, utoroshwaji wa wanyama hai, wizi wa nyara za serikali, ikiwamo pembe za ndovu, baadhi ya wananchi wamekuwa wakituhumu serikali kushindwa kuchukua hatua.

Vilevile, wananchi wamekuwa wakituhumu Serikali ya Kikwete, kukumbatia wezi wa fedha za umma katika halmashauri za miji na wilaya, uporaji wa ardhi unaofanywa na makampuni makubwa ya ndani na nje ya nchi.

Jana, Tanzania Daima Jumamosi haikufanikiwa kumpata Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu kuzungumzia iwapo serikali ina taarifa juu ya jambo hili kwa kuwa simu yake ilikuwa ikiita muda wote bila kupokelewa.

Kova ajivua
Kamanda wa Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam, Suleiman Kova jana ametangaza rasmi kujivua katika sakata zima la kuchunguza kutekwa na kuteswa kwa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari, Dk. Ulimboka.

Aidha, Kova pia amekanusha madai ya kuunda tume kuchunguza suala hilo, akitaka asiulizwe jambo lolote, huku akisukuma tukio hilo kwa wakubwa wake.

Juzi, Kamanda Kova aliliambia Tanzania Daima kwamba, jana angeweka wazi suala hilo ili Watanzania wajue kilichojiri kuhusiana na kutekwa na kuteswa kwa Dk. Ulimboka, jambo ambalo limetikisa anga, likiwemo lile la kukamatwa kwa raia wa Kenya, Mulundi anayedaiwa kuhusika na tukio hilo.

Hata hivyo, kinyume na matarajio ya wengi, jana Kamanda Kova aliruka kimanga na kudai kwamba wenye uwezo wa kulitolea maelezo ni wakuu wake wa kazi, kwa maana ya Ofisi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini.

Kuhusu kuundwa kwa kamati ya kuchunguza utekaji huo, Kova alisema kilichofanyika wakati huo ni kuundwa kwa jopo la uchunguzi ambalo taarifa zake hazina ulazima wa kutolewa mbele ya jamii zaidi ya kutumika kwa ajili ya utekelezaji wa kile walichokibaini.

Alisema baada ya kukamilisha kazi yake, alipeleka jukumu la kupeleleza sakata hilo katika ofisi ya mkurugenzi wa makosa ya jinai nchini (DCI) ambayo ndiyo yenye jukumu la kutoa maelezo.

Chanzo: Tanzaniadaima 12 Jan, 2013.
Sent from my BlackBerry® smartphone on the Tigo Tanzania Network

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.


--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 



--
www.wejobs.blogspot.com Jobs in Africa
www.jobsunited.blogspot.com International Job Opportunities

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment