Monday 17 December 2012

[wanabidii] TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU KIKAO CHA KAMATI KUU YA CHADEMA.

UFAFANUZI WA AWALI KUHUSU KIKAO CHA KAMATI KUU YA CHADEMA.

KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) iliyoketi kikao chake cha kawaida kwa siku mbili, Desemba 15-16, 2012, katika Hotel ya Blue Pearl, jijini Dar es Salaam, imemaliza kikao chake Desemba 16, usiku.

Pamoja na kwamba maazimio yote ya kikao hicho yatatolewa kwa umma kupitia vyombo vya habari, Desemba 18, 2012, huu ni ufafanuzi wa awali kutokana na kuwepo kwa taarifa zinazowakanganya wanachama na Watanzania kwa ujumla, zilizoandikwa tangu jana Jumapili na Jumatatu, katika baadhi ya vyombo vya habari.
Mbali ya kujadili masuala mbalimbali, ikiwemo kupokea taarifa ya hatua kadhaa za utekelezaji wa maazimio yatokanayo na vikao viwili vilivyotangulia, Kamati Kuu pia ilijadili hali ya siasa nchini, mchakato wa Katiba Mpya na Vuguvugu la Mabadiliko (M4C).

Kamati Kuu pia ilipokea taarifa ya mwenendo wa chama kutoka maeneo mbalimbali nchini, ambapo ilijadili pia kasoro za utendaji wa viongozi wa chama katika Wilaya ya Karatu.

Kamati Kuu ilichukua uamuzi wa kusimamisha uongozi mzima wa Wilaya ya Karatu na kuweka shughuli za utendaji wa chama chini ya uangalizi wa Kamati Kuu mpaka hapo itakapotolewa maagizo mengine baadae.
Aidha, Kamati Kuu pia ilipokea na kujadili mwenendo wa utendaji kazi wa baadhi ya viongozi wa taasisi za kiserikali wanaotokana na CHADEMA, hasa katika masuala ya ardhi na maji Wilayani Karatu.

Kikao pia kilibaini kuwa taarifa zinazohusu masuala hayo ya maji na ardhi ni tofauti na namna zilivyoripotiwa katika baadhi ya vyombo vya habari. Aidha kutokana na mjadala, iliazimiwa hatua kadhaa zichukuliwe, ambazo umma utaarifiwa katika tamko la Kamati Kuu litakalotolewa kupitia waandishi wa habari.
Imetolewa leo, Desemba 17, 2012, Dar es Salaam na;
Tumaini Makene
Ofisa Mwandamizi wa Habari CHADEMA



Sent from my BlackBerry® smartphone on the Tigo Tanzania Network

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com

DELL LATITUDE D 620 & D30

80 GB HardDisk ,CORE 2 DUO , 2.0 GHZ CPU ,1 GB RAM
DVD/CD - RW ,WINDOWS 7 /WINDOWS XP ,WIRELESS , BLUE TOOTH .

TSHS : 360,000 , 1 YEAR WARRANTY

CALL : 0786 806028
Free Delivery in Dar es salaam

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

0 comments:

Post a Comment