Sunday 23 December 2012

[wanabidii] Re: RAIS J.M.KIKWETE ANATAKIWA AMPISHE DR.SLAA IKULU

Dr Slaa hata kwenye kata anayoishi yeye mwenyewe hajapigiwa kura mwaka
2010

On Dec 23, 12:29 pm, GILL DAVID <gilldav...@yahoo.co.uk> wrote:
> Kama
> CCM inakubali kuwa Dr. Slaa ana kadi ya CCM na ni mwanachama hai basi
> Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete anapaswa apumzike kipindi hiki kilichobaki cha
> uongozi ampishe Dr Slaa aingie ikulu amsaidie kumalizia mda huu uliobaki
> kusafisha uchafu uliopo ndani ya chama na Serekali kwani yeye mheshimiwa
> Kikwete ameshindwa.Kama Dr Slaa aliweza kuwataja Mafisadi  pale Mwembe Yanga tuna imani naye zaidi kuwa
> ataweza kupambana nao kuliko Mheshimiwa Kikwete ambaye ametajiwa kabisa Wezi wa
> mali za Umma lakini anakaa nao meza moja na kula bila kuwachukulia hatua
> zozote.
>
>
>
>
>
> Watanzania
> wengi tungelijua hilo
> Mapema kuwa Dr Slaa anayo kadi ya CCM tungeandamana mheshimiwa Jakaya Mrisho
> Kikwete asiingie Ikulu kwani hata kwenye kura za uchaguzi vyombo vingi vya
> kusimamia uchaguzi kutoka nje ya nchi vilishatamka kuwa Dr Slaaa ndiye alikuwa
> anaongoza kwa kuwa na kura nyingi lakini Serekali ikachakachua matokeo. Uwezo
> wa kiutawala wa Dr
> Slaa ni bora mara mia moja kuliko wa mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete na ndio
> maana hata midahalo anaikwepa. Dr Slaa ndiye anafaa kuiongoza nchi mara dufu
> kulikoni JK.
>
>
>
> Ukiangali
> sana kila
> Kiongozo yeyote wa Upinzani wote wametokea CCM na kuanzisha vyama vingine. Wote
> lazima walikuwa na Kadi za CCM. Sasa inaelekea wengine walitupa kadi zao ama kwa
> kuwa walikuwa hawazilipii au pengine wanadaiwa na CCM kuzilipia kadi hizo jambo
> ambalo Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Nape Mnauye anatakiwa afuatilie madeni badala
> ya kupiga kelele hovyo kwa mtu aliyelipia kadi yake na hana deni kama Dr Slaa. CCM
> ni chama Mama wa vyama vyote. Hivyo mimi sioni sababu ya wao kupiga kelele eti
> Dr Slaa ana kadi ya CCM. Kadi ile inaweza kuwekwa kwenye jumba la Makumbusho ya
> chama cha CHADEMA kila mtu ajue jinsi gani Katibu wao alivyokuwa mwadilifu kwa
> kulipia kadi yake ya uanachama kwa miaka zaidi ya 20 kwa wakati mmoja.
>
>
>
> Serekali
> ya CCM ina tabia ya kuwafanya Watanzania kuwa wajinga na pengine wapumbafu.
> Nchi ina mjadala wa fedha zilizofichwa nje. Fedha ambazo zimeyumbisha uchumi mzima
> wa Taifa. Badala viongozi wa CCM na Serekali yake kujadili jinsi ya kuzirudisha
> fedha zile zisaidie kuongeza madarasa ya watoto wengi waliofaulu na hawana
> madarasa wao wanaingiza nchi kwenye mijadala isiyo na tija. Dr Slaa kuwa na
> kadi ya CCM hata kwenye pochi yake kunamuathiri nini mkulima na mfanyakazi wa Tanzania, au mtoto
> wa Kitanzania au mfanya biashara wa Kitanzania. CCM acheni mijadala isiyo na
> tija. Tumewachoka. Porojo mingi sana.
> Kama mnataka mbaki madarakani jadilini
> yafuatayo mjinusuru mwaka 2015.
>
>
>
> -Fedha
> zilizopatikana kwenye mashirika ya umma mliyoyauza ziko wapi?
>
> -Fedha
> zilizopatikana kwenye viwanda vya umma mlivyouza ziko wapi?
>
> -Fedha
> zilizopatikana kwenye wanyama mliowawinda na kuwauza nje ziko wapi?
>
> -Fedha
> zilizopatikana kwenye shamba za umma mlizouza ziko wapi?
>
> -Fedha
> zilizopatikana kwenye nyumba za umma mlizouziana ziko wapi?
>
> -Fedha
> zilizopatikana kwenye migodi ya umma zimefanyia kazi gani?
>
> -Fedha
> zilizopatikana baada ya kuuza Ranch za Taifa ziko wapi?
>
> -Fedha
> zilizofichwa nje ya nchi mnazirudisha lini ziongeze madarasa na maabara ya
> wanafunzi?
>
> -Fedha
> za mapato na matumizi ya Serekali ya miaka yote 51 mliyokaa madarakani lini
> mtaziweka wazi kwenye magazeti ya umma kama
> Uhuru, Mzalendo na Daily News.
>
> -Fedha
> zinazopatikana kwenye Hifadhi zetu za Taifa na Milima iliyopo Tanzania lini mtaziweka
> wazi kwa Watanzania?
>
> -Fedha
> mlizopata baada ya kuuuza ardhi ya Tanzania kule Loliondo lini
> mtaziweka wazi?.
>
> -Fedha
> mlizopata baada ya kuuza Bandari ya Mtwara lini tutazijua sisi Watanzania?
>
> -Fedha
> zilizopatikana baada ya kuwekeza Viwanja vyetu vya Ndege lini mtaziweka
> hadharani tuzijue?
>
> -Vitalu
> mnavyowinda wanyama mtatujulisha lini mapato yake?.
>
> -Mtatutajia
> lini Wabunge na Mawaziri wanaofanya biashara wakiwa kwenye nyadhifa za umma.
> Tunawajua wanaojenga mahoteli, wanaofanya biashara za mafuta, Usafirishaji nk.
>
>
>
> Mkiweza
> kuweka mambo haya bayana nina uhakika mtabaki madarakani vinginevyo 2015
> jitoeni tu wagombea wabaki ya vyama vya CHADEMA, CUF, NCCR, TLP, SAU nk. CCM
> Tanzania mmepoteza uelekeo na imani kwa Wananchi. Mkiona mtu anawashabikia
> labda ni mmoja wenu, au mpambe, au ana hisa na kampuni zenu, au ni muwekezaji,
> au mkwepa kodi, au mtoto wenu, au Zuzu, au mchumia tumbo, au anawapa mahirizi
> maana ndio zenu, au Mkweo, au Hawara, vinginevyo tumewachoka sana tu.
>
>
>
>
>
> Maswala
> ya kuongelea kadi ya Dr Slaa hayana tija kwetu. Tunataka muongelee yote niliyoyataja
> hapo juu tutawaelewa. Kumuongelea mtu anayependwa na Watanzania walio wengi
> mnapoteza mda wenu wakati tunajua kabisa ni wivu na husuda tu juu yake na
> alikuwa ameshinda uchaguzi wa 2010 mkamuibia kura.
>
>
>
> Mkereketwa
>
> Galliard
> David

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com

DELL LATITUDE D 620 & D30

80 GB HardDisk ,CORE 2 DUO , 2.0 GHZ CPU ,1 GB RAM
DVD/CD - RW ,WINDOWS 7 /WINDOWS XP ,WIRELESS , BLUE TOOTH .

TSHS : 380,000 , 1 YEAR WARRANTY

CALL : 0786 806028
Free Delivery in Dar es salaam

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

0 comments:

Post a Comment