Saturday 15 December 2012

Re: [wanabidii] Jamboleo, Mtanzania na Uhuru: Uwezo wa Waandishi na Wahariri wao.

Hizi habari hata mimi zimenishangaza sana. Hii ndio aina ya waandishi wanaoitwa pen prostitutes. Wanajali pesa zaidi kuliko utu na heshima na wataandika utumbo wowote watakaoletewa ilmradi mkono uende kinywani. Haya ni aina ya magazeti ambayo Dr Reginald Mengi huyaita vipeperushi. Kipeperushi hubeba ujumbe wowote autakao mtoaji wa kipeperushi husika. Uzuri ni kwamba magazeti kama haya ni ya msimu----uchaguzi ukishapita hutayaona mtaani----lengo la kuanzishwa kwao litakuwa ama limetimia au lime-fail. Magazeti haya hayaandiki habari ili yauze bali yanaandika ili kutimiza wajibu waliotumwa na mfadhili wao. Kwa hivyo, usishangae kwa nini haya magazeti hayanunuliki lakini kila siku yapo---kuna fungu limetengwa kwa ajili ya kuyawezesha yaendelee kutolewa kila siku. Habari ndio hiyo!


From: elias mhegera <mhegeraelias@yahoo.com>
To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
Sent: Saturday, December 15, 2012 11:28 AM
Subject: Re: [wanabidii] Jamboleo, Mtanzania na Uhuru: Uwezo wa Waandishi na Wahariri wao.

hizi ndiyo propaganda kwa ajili ya 2015 zimeanza

 
Elias Mhegera
Media & Information Officer 
Tanzania Human Rights Defenders Coalition 
Tel: 255-0754-826272
        255-0715-076272
Email: mhegeraelias@yahoo.com 
             mhegera@gmail.com 
The only thing we have to fear is fear itself 


From: Josephat Isango <joseisango@yahoo.com>
To: wanabidii@googlegroups.com
Sent: Saturday, December 15, 2012 4:04 PM
Subject: [wanabidii] Jamboleo, Mtanzania na Uhuru: Uwezo wa Waandishi na Wahariri wao.

Jamboleo, Mtanzania na Uhuru: Uwezo wa Waandishi na Wahariri wao.
 
Mwandishi unapoletewa stori ya BAVICHA, na mtu binafsi huulizi Maswali? Mbona kama BAVICHA ni suala pan asana, inakuwaje waandishi mnaitwa na mtu mmoja tu mkamsikiliza mkaandika mawazo yake mkaleta kwa watanzania? Msemaji wa BAVICHA, Ni Mwenyekiti wa BAVICHA kwa ngazi husika, kuanzia msingi, hadi Taifa. Waliotwa Mwanza na Katibu mmoja tu bila hata kuwa na Mwenyekiti wake, tena wanajua Katibu amesindikizwa na Mtu aliyefukuzwa Uanachama na Kamati Kuu akapoteza Udiwani, (Chagulani) na Edo Mwamalala aliyefukuzwa Uanachama na Kamati Tendaji ya Mbeya, pamoja na kundi jingine ambalo linatajwa kwenye mitandao kuwa lipo kazini, kwa pesa nyingi sana inayotolewa na baadhi ya watu tunaowafahamu kwa ajili ya Propaganda. mwandishi unapokuwa huulizi Maswali, unapeleka kwa Mhariri, stori ambayo kwanza hujabalance, halafu mnaiweka ukurasa wa mbele inatia shaka. Sijui pengine ndo mpango wa kufanya magazeti yenu yaache kuaminika. Kwa utaratibu huu, Waandishi na Wahariri mnajishusha chini kabisa kuliko kundi lolote katika jamii.
 
Hivi Mwandishi wa Mwanza, huwezi kumuuliza Mwamalala kwanini umekuja Mwanza toka Mbeya kufanya Mkutano na Waandishi huku kwenu hakuna? Huwezi Kumuuliza katibu mbona Mkutano huu ni wa kinyemela, Mwenyekiti wako yuko wapi? Imekuwaje wewe Utoke Mbeya, upite Dar, uje Mwanza kufanya Mkutano na waandishi, hivi Mikoa yote kwanini umepita? Iringa, Morogoro, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga, Simiyu hadi Ukaja huku na ukashirikiana na Katibu tu, ndo huyu amekusababisha utoe nauli toka Mbeya kuja kuongea naye, si mgeongea kwa simu tu kila mmoja akatoa tamko?. Hii BAVICHA ya watu wawili ikoje?. Baadhi ya Waandishi na Wahariri Uwezo wao nadhani hata ndani ya familia zao wanautilia shaka, sijui kwenye jamii.
--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
DELL LATITUDE D 620 & D30
 
80 GB HardDisk ,CORE 2 DUO , 2.0 GHZ CPU ,1 GB RAM
DVD/CD - RW ,WINDOWS 7 /WINDOWS XP ,WIRELESS , BLUE TOOTH .
 
TSHS : 360,000 , 1 YEAR WARRANTY
 
CALL : 0786 806028
Free Delivery in Dar es salaam
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 


--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
DELL LATITUDE D 620 & D30
 
80 GB HardDisk ,CORE 2 DUO , 2.0 GHZ CPU ,1 GB RAM
DVD/CD - RW ,WINDOWS 7 /WINDOWS XP ,WIRELESS , BLUE TOOTH .
 
TSHS : 360,000 , 1 YEAR WARRANTY
 
CALL : 0786 806028
Free Delivery in Dar es salaam
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 


0 comments:

Post a Comment