Saturday 20 October 2012

[wanabidii] KIZAZI HIKI NI CHA KUDADISI!

Katika Biblia mke wa Nuhu aliambiwa asiangalie nyuma wakati wa kuingia kwenye Safina. Akaangalia kijanja akawa jiwe LA CHUMVI.

Watoto wa siku hizi ukimwambia usishike umeme, utakufa, atashika ili aone kama atakufa. Na kama hatakufa ile shock itamfunza asirudie tena.

Misahafu ni vitabu vitakatifu. Vinatakiwa viheshimiwe na vitunzwe vizuri. Ni vema kuwafundisha watoto wetu kuviheshimu na kuvitunza.

Tukiwaambia ukikiharibu utalaaniwa na Mungu. Mwanzo ataogopa maana hajui maana ya laana ni nini. Kadiri ya kukua na udadisi wake ataelewa pole pole maana ya laana.

Ukimwambia ukikikanyaga utakuwa mbuzi siku moja akiwe mwenyewe atakikanyaga ili aone kama atakuwa mbuzi. Asipokuwa mbuzi ni hatari ya kukidharau kwa kuona kile alichofundishwa ni uwongo amedanganywa na hakuna ukweli.

Wazee wetu pia walifundishwa mwanamke mjamzito asile mayai kwa vile atazaa mtoto asiye na nywele. Siku hizi wanakula. Katika kabila langu tukiwa watoto tuliambiwa tusile nyama ya maini maana utakapo tahiriwa utatoka damu nyingi. Siku hizi wanakula. Kumbe mafundisho yale yalikuwa UWONGO. 

Tuangalie Elimu tunayowarithisha watoto wetu. Inaweza kuwapotosha.

0 comments:

Post a Comment