Wednesday 10 October 2012

Re: [wanabidii] ISMAIL JUSSA NA ZANZIBARI HURU.

safi sana huyu

2012/10/10 Mohamedi Mtoi <mouddymtoi@gmail.com>

Kwenye facebook wall yake ameandika hivi:

"Wakati tunaelekea India wiki iliyopita tukiwa Uwanja wa Ndege wa Dubai wakati tunabadilisha ndege, tulikutana na mmoja wa Makamishna wa Tume ya Katiba kutoka upande wa Tanganyika ambaye ni msomi wa hali ya juu.

Katika majibu ya kustaajabisha wakati nilipomuuliza vipi hali ya utoaji maoni inaendelea, alitujibu kuwa inaendelea vizuri na pamoja na kwamba upande mmoja (nna hakika alikusudia Zanzibar) unatoa madai makubwa, yeye haimpi tabu kwa sababu anajua wanaofanya hivyo wanajipa nafasi kubwa ya kuja kupatana (alitumia neno la Kiingereza 'bargaining') ili kupata muafaka wa kati na kati.

Bahati mbaya mawazo kama haya ya Kamishna huyu ndiyo mawazo mgando ya watunga sera na sheria wengi wa Tanganyika wanaojiona kama ni watawala au wamiliki wa Zanzibar na hivyo kujipa matumaini kuwa Zanzibar tunaposema tunataka kurejesha mamlaka yetu kamili kitaifa na kimataifa tukiwa na kitu chetu Umoja wa Mataifa huwa tunatafuta 'kupatana' au kwamba hatuna uwezo huo mpaka Tanganyika waridhie.

Wanapaswa wajue sasa kabla hawajachelewa kwamba mamlaka kamili ya Zanzibar (Sovereign Zanzibar) siyo ombi ni matakwa ya Wazanzibari na tutayasimamia kwa nguvu na uwezo wetu wote. Na katika kulifikia lengo hilo hakuna wa kutuzuia isipokuwa Mwenyezi Mungu. Pamoja Daima!"

Huyo ndiyo Jussa Ismail.
Sent from my BlackBerry® smartphone on the Tigo Tanzania Network

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.





--
Bariki G. Mwasaga,
P.O. Box 3021,
Dar es Salaam, Tanzania
+255 754 812 387

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment