Wednesday 12 September 2012

[wanabidii] Dr. Kafumu Apata Ajali Jimboni Igunga

Dr. Dalaly Kafumu amepata ajali ya kupinduka na gari akielekea kwenye kijiji kimoja kilichopo kata ya Mwisi ambako alikuwa anaelekea kushiriki mazishi ya Mama mmoja maarufu. Ajali hiyo ilitokea jana ambapo gari ilipoteza uelekeo kutokana na hitilafu ya barabara na hivyo kuvutwa, kugonga gema na kupinduka mara moja na gari kukaa matairi juu.

Gari iko nyang'anyang'a huwezi amini kama kuna mtu ametoka salama, lakini tunavyoongea hapa Dr. Kafumu na kijana wake ambaye alikuwa akiendesha walitoka salama. Dk. Alibanwa na Airbags na walilazimika ili kumtoa kuvunja mavyuma kwa shooka na kumkuta amezimia na alizinduka baada ya muda kidogo, pia alikuwa na bruises zilizokuwa zinavuja damu sana kichwani na alilazwa hospitali ya Nkinga na asbh hii atapewa ruhusa arudi nyumbani.

Amekuwa jimboni humo toka Jumatatu akifanya ziara ya kukamilisha miradi ya maendeleo aliyoianzisha, pia kuwaondoa mashaka wananchi kuwa hatowatelekeza kwa kuwa ametolewa Ubunge, na kwamba bado yuko nao pamoja tu.
Sent from my BlackBerry® smartphone from Vodacom Tanzania

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

0 comments:

Post a Comment