Thursday 27 September 2012

Re: [wanabidii] Zitto: Ubunge sasa basi - Mwanzo

Zitto kweli anaweza kuwa rais na anao uwezo na pia katiba ya nchi
pamoja na chama chake cha CHADEMA vinatoa mwanya huo kama kweli ana
nia ya dhati. Tatizo ninaloliona hapa ni mahali na namna anavyotangaza
nia yake, anaonekana kama kuna kitu anakiogopa au kiko nyuma ya pazia
(something fishy). Hii ni mara ya pili kumsikia akitangaza nia hiyo
kwa utaratibu kama huo.

Kwa vile chama chake kinao utaratibu wa kufuata ingekuwa vyema kama
ataanza kutangaza nia hiyo kupitia chama chake ili apate kuungwa mkono
na ngazi za chama kabla ya kuutangazia umma moja kwa moja? Sijui
anafanya pilot test au anataka kupata nguvu ya umma ili Chadema
wakikataa kumpitisha umma umpe support? Anaposema Ubunge basi ana
maana gani kama kweli bado ana nia ya kuuendeleza upinzani? Anajua
fika kwamba kwa nchi za dunia ya tatu kuking'oa chama tawala ni sawa
na kuung'oa mbuyu, inakuwaje aone ni rahisi kugombea na kuupata huo
urais na hivyo kuachana na mambo ya ubunge?
Akumbuke hata huo ubunge si mwepesi kuupata maana uchaguzi uliopita
(2010) alimzidi mpinzani wake kwa kura kidogo tu ukilinganisha na
kipindi kilichopita(2005) alipokuwa amemzidi mpinzani wake kwa mbali
sana.Sijui anapata wapi nguvu ya kujiamini kuupata huo urais na
kuachana kabisa na ubunge wakati upepo wa siasa kwake haujakaa vizuri
sana (the trend is not out of doubt).

Mimi namshauri wakati anapopanga kugombea urais ni vyema akajiimarisha
katika ngazi zote za chama toka ngazi ya chini hadi ya juu kabisa. Pia
namshauri aachane na wazo la kuundoa ubunge akilini mwake maana
amefanya kazi nzuri na bado tungependa aendelee kuwemo bungeni na
kuuimarisha zaidi upinzani. Kitendo cha kusema ubunge basi kinaonyesha
kama vile anajua fika anakubalika vya kutosha kwa wapiga kura na hivyo
urais must. Ndugu zangu wa Kigoma jimbo hilooo limetangazwa anza
kuchangamka mapema bahati yaweza kuwa yako tangaza nia mapema kama
alivyofanya zitto kwenye nafasi ya urais.

2012/9/28 samson charles <samchaz307@gmail.com>:
> naamini.............. anaweza
>
>
> 2012/9/28 John George <georgejn2000@gmail.com>
>>
>>
>> Nampa hongera Mh. Zitto kwa uamuzi huo. Anaweza kuwa Rais
>>
>> 2012/9/28 Magiri paul <kiganyi@gmail.com>
>>>
>>> "Nimefanya kazi kubwa katika kazi yangu ya ubunge, nimeleta mabadiliko
>>> mengi kuanzia bungeni mpaka jimboni. Nadhani inatosha na hata nikiongezewa
>>> miaka mingine sitaweza kufanya yale yaliyonishinda katika kipindi cha miaka
>>> kumi. "Kama Mungu ataniweka mpaka mwaka 2015, sitagombea ubunge tena kwa
>>> sababu kazi niliyofanya inatosha. Natangaza rasmi kuwa nitagombea urais
>>> kupitia chama changu cha Chadema, bila kusababisha msuguano wowote na sitaki
>>> kuingia katika historia ya kurudisha nyuma harakati za upinzani kushika
>>> dola," alisema Zitto.
>>> http://wotepamoja.com/archives/7516#.UGUpr1ZTOfU.gmail
>>>
>>> --
>>> Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
>>> Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
>>> Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
>>>
>>> Kujiondoa Tuma Email kwenda
>>> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha
>>> ukishatuma
>>>
>>> Disclaimer:
>>> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any
>>> legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts
>>> must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you
>>> agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
>>>
>>>
>>
>>
>> --
>> Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
>> Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
>> Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
>>
>> Kujiondoa Tuma Email kwenda
>> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha
>> ukishatuma
>>
>> Disclaimer:
>> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal
>> consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be
>> presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to
>> this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
>>
>>
>
>
> --
> Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
> Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
> Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha
> ukishatuma
>
> Disclaimer:
> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal
> consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be
> presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to
> this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
>
>

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

0 comments:

Post a Comment