Monday 24 September 2012

Re: [wanabidii] Uhamiaji wanafanya nini? Kumbe Hussein Bashe si Raia!

Mambo ya aibu kabisa! Vita ya kisiasa inakuwa kama personal. Watu wako obsessed na character assasination na hawaoni jingine la maana la kufanya kwa ajili ya nchi yao.
 
Sio juu yangu kuamua kuwa Bashe au Bashir ni raia au sio raia lakini huu utumiaji wa uraia kama silaha ya maangamizi kwa wapinzani wenu wa kisiasa ni mtego wa panya. Yeyote aushangiliae mpeni pole!!!!
2012/9/24 paul lawala <pasamila292000@gmail.com>
Vita vya makundi ndani ya CCM au?

Mbona kila uchaguzi ukija ndiyo Tunasikia habari za uraia?

Au ndiyo zile siasa zinazoitwa "maji taka"

2012/9/24 Gwaigwa Maduhu <gmaduhu@gmail.com>:
> Maganga Masanja,
> NZEGA.
> TABORA
> +255786731566 (DSO)
> 18th Sept. 2012
>
> Katibu Mkuu,
> Chama Cha Mapinduzi Makao Makuu DODOMA.
>
> Mheshimiwa,
>
>
>
>
> Yah: Taarifa Kuhusu Ndugu Husein Mohamed Bashe
>
> Tafadhali husika na kichwa cha barua hii hapo juu.
>
> Mimi ni mkazi wa Nzega na ni mwanachama hai wa CCM hapa Nzega. Nimeshuhudia
> na kusikia mengi yakisemwa kuhusu wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi
> katika chama hapa Nzega nikaona ni vyema kama mwanachama na kama raia mwema
> nikatoa taarifa nilizonazo ili mzifanyie kazi wakati mkiwajadili wagombea wa
> nafasi mbalimbali na pia mkajiridhisha kuhusu taarifa hizi ili mfanye
> maamuzi yanayofaa kwenye vikao vyenu. Mimi nimefuatilia swala hili kwa
> kusoma maelezo aliyoyachapisha Huseni Bashe kwenye mitandao na pia kuongea
> na baadhi ya wazee wa hapa mjini Nzega(walioipokea familia ya shehe Mohamed
> Ibrahim na mkewe) na kubaini ukweli ufuatao, pia nimesoma sheria ya
> uraia(The Tanzania citizenship act, principal legislation, Chapter 357
> revised edition, 2002)
>
> Ndugu Husein Mohamed Bashe ama Husein Mohamed Ibrahim Bashir (tunashangaa
> kwa nini jina lake limekuwa likibadilika badilika – wengine wakidhani ni
> katika kutafuta uhalali wa kujiita Mnyamwezi kama nyaraka zake za kughushi
> Uraia zinavyoonyesha), ambaye anajulikana hapa Nzega kama mtoto wa Shehe
> Mohamed Ibrahim, alizaliwa Nzega Mnamo Tarehe 26/08/1975 (kumbukumbu rasmi
> za kuzaliwa kwake zinapatikana Ofisi ya Vizazi na Vifo, Nzega - kwenye cheti
> chake cha halali cha kuzaliwa; Shule ya Msingi Kitongo, Nzega, aliposajiliwa
> darasa la kwanza Mwaka 1984; na Chuo Kikuu Mzumbe alipodahiliwa kuanza
> masomo ya shahada ) na wazazi wake wote wawili wakiwa wasomali pure kutokea
> Somalia, na wote hawa hawakuwa Raia wakati Huseni akizaliwa. Baba yake
> Husein amepata Uraia 1987 kwa taratibu za kuomba kisheria. Mama yake Huseni
> anayejulikana kwa jina la Zainab Abdi hajawahi kuwa raia wa Tanzania na
> hajawahi kuomba na kupewa Uraia (hivyo anaishi nchini kinyume cha sheria).
>
> Kwa kuwa wazazi wote wawili wa Huseni hawakuwa raia wakati wanamzaa yeye na
> wadogo zake wote watano kwa mujibu wa sheria wote hawa si raia na wako ndani
> ya Tanzania kinyume cha sheria.
>
> Kama raia mwema nimepata taarifa kwamba kuna mtandao wa wasomali ambao
> wameingia nchini siku hizi na wametengeneza genge la kutafuta uhalali wa
> kuishi nchini hapa na kutawala nyanja mbalimbali za uchumi na jamii na hivyo
> nikahofia kwamba isije kuwa ndugu Huseni naye ni mmoja wapo uki zingatia
>
>
> amekuwa akifanya jitihada za kina na kwa kutumia nguvu kubwa sana ya pesa
> (ambazo hatujui anazipataje ukilinganisha na hali ya maisha ya familia yake
> na wazazi wake hapa Nzega) kutafuta ubunge na uongozi ndani ya chama tawala.
> Wengine hapa Nzega wamekuwa wakisema kwamba anatafuta ubunge kwa nguvu namna
> hii ili ahalalishe uraia wake wa uongo alionao na atafute namna ya kuingiza
> ndugu zake nchini Tanzania kwa kutumia nguvu ya kisiasa. Watu wengi wamepata
> mashaka hapa Nzega na kuna minong'ono kwamba anafadhiliwa na huo mtandao wa
> kiharamia wa kisomali wenye nia ya kutafuta namna ya kupenyeza watu wao
> kwenye system. Hili hasa ndiyo limenitisha na kunifanya niamue kutoa taarifa
> hii ili vyombo vya dola vilifanyie kazi na ukweli uthibitike.
>
> Mwaka 2005 aligombea Ubunge na alipewa alama ya D kwa sababu ya 'utata' wa
> Uraia wake.
>
> Mwaka 2008 aligombea uenyekiti wa UVCCM Taifa na vikao vilimjadili na
> kuonyesha utata kwenye uraia wake, na hapo alikimbia kutengeneza kiapo cha
> kugushi cha haraka haraka cha kuthibitisha uraia wake.
>
> Watu wengi, na mimi nikiwemo tulibaki na mashaka yetu kwamba ni katika
> mazingira gani mtanzania wa kuzaliwa atalazimika kula kiapo kuthibitisha
> uraia wake? Hivi ni wangapi kati yetu wamewahi kufanya hivyo? Kwangu hili
> limekuwa likinipa mashaka makubwa na kunifanya niamue kufanya ufuatiliaji wa
> kina.
>
> Mwaka 2010 aligombea ubunge na alikatwa jina na vikao vya juu vya CCM kwa
> sababu ile ile ya 'utata' kwenye uraia wake. Mwaka 2010 Waziri wa Mambo ya
> ndani Laurence Masha alithibitisha kwenye vyombo vya habari kuwa ndugu
> Huseni Bashe ni raia japokuwa hapa Nzega ambapo wanamfahamu ndugu huyu na
> chimbuko la familia yake toka wanaingia walibaki na mashaka yao. Hali hii na
> wasiwasi nilionao juu ya mtandao huu vimenifanya kuandika waraka huu ili
> kukiomba chama kitupe ukweli wa swala hili ni nini na pengine kumtaka Huseni
> Bashe, mama yake na wadogo zake wafuate taratibu za halali za kutafuta uraia
> wao.
>
> Hata hivyo pamoja na waziri wa mambo ya ndani kutoa uthibitisho huo kwenye
> vyombo vya habari hakumpa ndugu Huseni Bashe hati yoyote ile ya kumpa Uraia.
> Hivyo maneno yale yanabaki kuwa kauli ya kisiasa isiyo na mashiko yoyote
> yale kisheria kwa mujibu wa sheria hiyo niliyoitaja hapo juu.
>
> Kwa kuwa baba yake alipewa uraia tarehe 27/05/1987 baada ya kuishi kwa hati
> ya ukazi kwa muda mrefu na kuamua kuomba uraia na kufuata taratibu zote
> hakuna utata kwamba alikuwa raia wa Somalia kwa muda wote kabla ya hapo.
> Hata Huseni mwenyewe amejaza kwa kuthibitisha hili kwenye fomu yake ya
> kugombea Ubunge kuwa baba yake alizaliwa mwaka 1947 sehemu inayoitwa Buroa,
> Mkoa wa Buroa kule Somalia. Japokuwa maelezo yaliyopo kwenye mtandao
> aliyoyatoa kumshambulia mbunge wa nzega mheshimiwa dr. Kingwangallah
> anaandika hadithi tofauti kwamba baba yake alizaliwa Tabora mjini.
>
> Uraia wa mama yake unabaki kuwa ni swala lenye kuhitaji uchunguzi na
> uthibitisho. Huseni hutoa maelezo ya kwamba mama yake ni mnyamwezi wa Tabora
> jambo ambalo halikubaliki maana hata Kiswahili, achilia mbali kinyamwezi,
> hakifahamu vizuri na pia hata muonekano wake ni wa kisomali bila shaka
> yoyote. Kwa maelezo ya Husein Bashe kwenye andiko la kashfa kwa mbunge wa
> nzega dr. kingwangallah anadai kuwa wazazi wa mama yake ni wazaliwa wa
> Tanzania, Sumbawanga (Baba yake na Mama Husein) na Boma Ng'ombe (bibi yake
> na mama Husein) kwamba walichagua uraia wa Tanzania
>
>
> kutoka ule wa Somaliland wakati wa Uhuru lakini hakuna kumbukumbu hata moja
> kuwa waliandikwa kwenye rejista ya raia wa Tanzania waliosajiliwa kama
> 'aliens' kwa mujibu wa sheria iliyokuwa inatambua uraia wa kuandikishwa,
> yaani 'citizenship by registration' ya watanzania minorities wakati tukipata
> uhuru. Habari hizi zinaonekana ni za uongo kwa kuwa tayari tuna ushahidi wa
> cheti cha kugushi cha mama yake na mama Husein Bashe (aliyejulikana kwa jina
> la Amina bint Ahmed) na tuna taarifa kwamba babu yake kizaa mama na Husein
> alitokea kijiji cha Belibeli kule Somaliland akiingia Tanzania na mkewe bi
> Amina na watoto (akiwemo mama Husein – Zainab bint Abdi).
>
> Alichokifanya Huseni Bashe ili apate Uraia
>
> Kwa mujibu wa sheria ili upate uraia wa Tanzania ni lazima uwe umeishi
> nchini kwa kibali cha ukazi na umeishi kwa kipindi kisichopungua miaka 10,
> saba kati ya hiyo uwe umeishi mfululizo huku ukiwa mwema na mwenye faida kwa
> nchi kijamii ama kiuchumi (second schedule, conditions for citizenship by
> naturalization, section 9(1) ya sheria niliyoitaja hapo juu) . Na maombi
> hayo yanaanzia kwenye kata unayoishi (kanuni namba 8 iliyomo kwenye Tanzania
> citizenship regulations (section 28)) pia alitakiwa mwombaji (Huseni Bashe)
> kutangaza kwenye magazeti ya kila siku kwa siku 2 zinazofuatana (kanuni ya
> 3 ya kanuni nilizozitaja hapo juu). Mpaka naandika hapa hakuna gazeti wala
> mtu hata mmoja katika
> niowahoji aliyekumbuka kuona tangazo la namna huyo kumhusu Husein Bashe.
>
> Kwa kufuata utaratibu huu unaoelekezwa na sheria na kanuni zake alijua
> angepoteza matumaini ya kuingia kwenye siasa mapema na ingewezekana kuwa
> ndiyo ukomo wake kabisa. Aliamua kutafuta njia fupi ya kupata uhalali wa
> uraia wake kwa kugushi hati za kuzaliwa za mama yake mzazi na za bibi yake
> kizaa mama (ambazo naziambatanisha hapa). Kwa kufanya hivi alijua atapata
> uhalali wa kutumia kipengele cha sheria kinachosema kama mzazi wako mmoja ni
> mtanzania na wewe umezaliwa Tanzania basi unaukana tu uraia wa mzazi mmoja
> ambaye hakuwa mtanzania wakati unazaliwa. Hivyo alipata mwanya wa kuukana
> uraia wa baba yake na kudai amebaki na uraia wa mama yake (ambaye alidai
> kuwa ni mnyamwezi na hata kwenye hati ya Husein Bashe inaonekana hivyo).
>
> Hati ya kuzaliwa ya mama yake mzazi na Husein Bashe ninayo kivuli chake na
> nitakiambatanisha na barua hii pia cha bibi yake. Vyeti vyote hivi ni vya
> kugushi na hili tumelithibitisha RITA. Cheti cha mama yake Huseni Bashe kina
> taarifa zifuatazo:- No. of Entry 3032, Namba ya cheti A. 17404 na
> kimesainiwa na L. M. Manson tarehe 14/02/1984, kimetolewa wilayani Tabora,
> na kinadai mama yake Husein Bashe, mwenye jina la Zainab bint Abdi alizaliwa
> Government European Hospital na ni wa kabila la Isihakia kutokea Somalia. Na
> kile cha Bibi yake Husein Bashe kina No. of entry 3508, na namba ya cheti A
> 17399, na kimesainiwa na A. B. Hodgson, kimetolewa wilaya ya Moshi tarehe
> 14/02/1984, amezaliwa Boma la Ng'ombe, na jina lake ni Amina Binti Abeid, na
> ni wa kabila la Isihakia. Jambo la kuvutia ni kwamba kwenye vyeti vyote hivi
> aliyesaini ni mtu mmoja (japokuwa ni mikoa miwili tofauti na siku moja).
>
> Mbali na RITA kukana kutokuvitambua vyeti hivi kuna kila alama ya kugushi
> kwenye nyaraka hizi kwanza vyote vimesainiwa na kutolewa siku moja, na mtu
> mmoja kwenye mikoa tofauti na serial number za kufuatana (17404 na 17399!)
> pia walioandikwa kusaini wana majina tofauti yanayoonesha kuwa ni foreigners
> (Manson na Hodgson). Watu wenye majina hayo hawajawahi kuwepo Tabora wala
> Moshi. Pia hakujawahi kuwa na hospiali yenye jina hilo lililotajwa hapa
> Tabora na ni kitu kisichowezekana kwa ofisa
>
>
> wa serikali kukosea jina la Boma Ng'ombe na kuandika Boma la Ng'ombe pia
> kuandika kwamba ipo
> wilaya ya Moshi badala ya wilaya ya Hai.
>
> Uchunguzi wangu umebaini kuwa mama yake hakuzaliwa Tanzania na kwamba
> aliingia Tanzania kupitia Rundugai akiambatana na wazazi wake na wajomba wa
> Huseni Bashe (mmoja yupo Dodoma – maarufu kama Charles mnene, na ambaye
> alinipa historia hii bila kujua ninachokifanya) wakati huo mama yake mzazi
> Husein akiwa na umri wa miaka 8/9.
>
> Alitafuta njia fupi ya kujipatia uraia ili kukwepa mlolongo wa taratibu kwa
> sababu za kisiasa. Kiuhalali – alitakiwa alipofikisha umri wa miaka 18 aanze
> kuishi kwa kibali cha ukazi kwa kipindi cha miaka 10 ndipo afanye maombi
> yake rasmi ya kupatiwa Uraia jambo ambalo lingemnyima sifa ya kugombea
> uenyekiti wa UVCCM Taifa mwaka 2008, hivyo alikwepa akapita njia fupi. Sasa
> kwa kufanya hivyo amevunja sheria kwa kugushi nyaraka za uraia za mama na
> bibi yake na ana kosa la kujibu kisheria, yeye na pamoja na bibi na mama
> yake.
>
> Anachotakiwa kufanya kwa sasa kuhusiana na Uraia wake
>
> Anatakiwa kuomba kibali cha ukazi na aishi kwa kipindi cha miaka 10, 7 kati
> ya hiyo ikiwa ni ya mfululizo na akiwa ni mtu mwema na mwenye faida kwa nchi
> kijamii na kiuchumi ndipo afanye upya maombi ya uraia.
>
> Tabia ya kugushi nyaraka na taarifa mbalimbali
>
> Amekuwa akidanganya umri wake kwa kuwa na siku mbalimbali za kuzaliwa –
> ushahidi ni taarifa alizojaza kwenye fomu mbalimbali za kugombea nafasi za
> Uongozi kwenye chama, mfano mwaka 2005 alipogombea ubunge alijaza amezaliwa
> mwaka 1976, mwaka 2010 alipogombea ubunge alijaza kuwa amezaliwa mwaka 1978.
> Pia mwaka 2007 alikuwa anagombea Ujumbe wa Halmashauri kuu ya Mkoa alijaza
> kuwa amezaliwa mwaka 1977. Siku yake ya kuzaliwa imekuwa ikibadilika
> badilika kutokana na mahitaji ya wakati huo. Siku yake ya kuzaliwa
> ilibadilika ili apate fursa ya kugombea UVCCM mwaka
> 2008 (kwa kushusha umri wake akidhi vigezo) na tarehe hiyo inapatikana pia
> kwenye kiapo chake cha
> Uraia anachotumia (hivyo nacho ni batili) na pia kwenye kitambulisho chake
> cha mpiga kura (kama inavyoonyesha kwenye daftari la kudumu la wapiga kura).
> Ukitaka kuamini kuwa amedanganya umri linganisha taarifa hizi na za mdogo
> wake aliyemuachia ziwa anayejulikana kwa jina la Ismail Mohamed, ambaye naye
> amezaliwa mwaka huo huo wa 1978. Kiapo chake cha uraia kilipatikana tarehe
> 24/09/2008 akiwa na umri wa miaka 30, umri ukiwa ni wa uongo kwa kuwa
> alikuwa amefoji vyeti vya kuzaliwa.
>
> Pia mwaka 2005 akigombea Ubumbe aliandika kuwa ana digrii mbili, ya kwanza
> ya Mzumbe nay a pili
> (MBA) ya UNISA, ambayo hakuwa nayo na mpaka leo hii hana.
>
> Pia amewahi kufukuzwa kazi sehemu mbalimbali kwa udanganyifu:- alidanganya
> NMB benki kuwa anaumwa kumbe amelala nyumbani kwa uvivu wa kwenda kazini.
> Bosi wake alipozidi kumtafuta na aliposikia kuwa kuna hatari ya kufukuzwa
> kazi aliamua kutafuta daktari wa uongo ili amfunge POP ndipo akaenda
> kuripoti huku akiwa anatembea akichechemea kwa msaada wa magongo mpaka kwa
> bosi, watu wakampa pole nyingi pale ofisini. Alipoingia na kumueleza bosi
> wake kuwa hakuja kazini kwa sababu
>
>
> alivunjika mguu bosi alimhoji kwa nini hakuchukua seek sheet na kwa nini
> hakutoa taarifa, akashindwa kujibu. Pamoja na hali aliyokuwa nayo bosi
> aliamua kumkabidhi barua ya kumfukuza kazi; Husein alilia sana na kisha
> akatupa magongo akaondoka bila kuchechemea tena kama alivyoingia. Watu
> wakashangaa na kuangua vicheko. Pia amewahi kufukuzwa kazi pale Celtel kwa
> kosa la uzembe na kutokuweka sawa hesabu zake. Amewahi kufukuzwa kazi kwa
> tuhuma za matumizi mabaya ya pesa na kampuni nyingine ya wazungu wa Afrika
> Kusini iliyokuwa inatengeneza kadi za mabenki.
>
> Haya ni baadhi ya mambo niliyoweza kukusanya dhidi ya mtu huyu ambayo
> nadhani mnahitaji kuyajua ili kuwasaidia kufanya maamuzi sahihi. Je ni kweli
> Tanzania inahitaji kuongozwa na vijana wa namna hii?
>
> Natanguliza shukrani zangu za dhati nikitarajia mtu huyu atapata
> anachostahili. Wako mtiifu,
>
>
> Maganga Masanja (kwa sababu za kiusalama nimeficha jina halisi ila ukitaka
> kunipata kwa maswali ama kwa ushahidi fika kwa DSO Nzega na mimi
> nitajitambulisha pale)
> Mwanaccm Mwaminifu, Nzega.
>
>
>
>
> Nakala:
>
> 1. Mwenyekiti wa CCM – Kwa taarifa
> 2. Naibu Katibu Mkuu, Mh John Chiligati (Mb.) – kwa ufuatiliaji (maana
> amekuwa akikutaja kwenye hotuba zake kwamba ulimsingizia kwa chuki zako)
> 3. Mwenyekiti wa CCM (M) Tabora – kwa taarifa
> 4. Katibu wa CCM (M) Tabora – kwa ufuatiliaji na uthibitisho
> 5. Mkurugenzi Mkuu Usalama wa Taifa – kwa uchunguzi wa kina na uthibitisho
> 6. Mkurugenzi Mkuu TAKUKURU – kwa uchunguzi wa kina na uthibitisho
> 7. Msajili wa vyama vya siasa – ndugu John Tendwa – kwa ufuatiliaji wa hatua
> zitakazochukuliwa na chama cha mapinduzi
> 8. DPP – kwa upelelezi na hatua za kisheria
> 9. DCI – kwa upelelezi na hatua za kisheria
> 10. Kamishna Mkuu Uhamiaji – kwa upelelezi na hatua za kisheria
> 11. Waziri wa mambo ya ndani ya nchi – kwa taarifa
> 12. Uhamiaji, Nzega – kwa taarifa
> 13. Usalama wa Taifa, Nzega – kwa taarifa
> 14. Mbunge Nzega – kwa taarifa
> 15. DC Nzega – kwa taarifa
> 16. CCM Nzega – kwa taarifa
>
> --
> Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
> Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
> Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha
> ukishatuma
>
> Disclaimer:
> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal
> consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be
> presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to
> this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
>
>

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.





--
Wasalaam
 
Denis Matanda,
Mine Supt,
Nzega - Tanzania.
 
" Low aim, not failure, is a crime"

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment