Saturday 18 August 2012

Re: [wanabidii] Re: Nani anapaswa Ku-update website ya Serikali

Afisa habari au uhusiano hiyo ndo kazi yake,in short afisa huyu lazima awe na upeo wa web designing na lazima kila siku apitie siyo website pekee bali pia masanduku ya maoni na kupitia pia wateja wanaopata huduma pale wanasemaje na zaidi ya yote wafanyakazi kujua nini kero zao na kuishauri management au wizara nini cha kufanya,but huko mawizarani na taasisi nyingi za serikali,hizi job description unakuta hawa maafisa habari kazi zao mara nyingi ni kupitia magazeti na kugeuka kuwa mamesenja kuzunguka na madokezo sabili toka idara ya sera na mipango hadi uhasibu,na government communication etc na kusahau wito wa taaluma hii mwisho wa siku,utakuta afisa habari anabaki anahengi na kubaki kuwa kama kituko wizarani hana ubunifu hapewi nafasi ya kuonesha kipaji chake,wengi ukiwauliza hawa makatibu wakuu na wengine wa wizara utakuta wanakujibu.....................aaaaaaaaah hao ni watu wa magazeti na kuchukua maswali kwa waandishi na kumpelekea mwandishi.....dah,Tanzania ipo siku itafunguka lakn kwa sasa bado sana,pamoja na semin a elekezi,hapo utakuta tunaingia gharama kuajiri mtu wa IT kudeal na website,sawa lakn afisa habari anahitaji maelekezo kidogo tu kutoka kwa mtu huyu kila kitu kitakuwa sawa.........ni swala la muda na kuwa na maafisa utumishi wanaojitambua na wenye weredi wa kutofanya kazi kwa mazoea na kuamua kufanya kama taaluma inavyoelekeza sio siasa inavyotaka......naelekeza tu.

From: Yona F Maro <oldmoshi@gmail.com>
To: Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
Sent: Saturday, August 18, 2012 7:45 PM
Subject: [wanabidii] Re: Nani anapaswa Ku-update website ya Serikali

ni vizuri tukajua kwanza nani ana manage hii tovuti ya serikali
tanzania.go.tz , maana unaweza kukuta ni mtu mmoja aliyesajili sehemu
fulani na yeye ameacha kazi hapo kila kitu kikafa , ukiuliza tznic
unaweza kupata taarifa zaidi , pia nadhani tovuti ya serikali
haitakiwi kuwa na kila kitu kunatakiwa kuwa na vitu vya muhimu tu
vingine vyote vishuke kwenye idara za serikali na zisomwe hapo kwa
njia ya feed kila zinapofanyiwa maongezeo mbalimbali .

mwisho napenda kusisitiza haya ya idara za serikali ku Outsource
shuguli kama hizi kwa kampuni nyingine zinazoweza kufanya shuguli hizi
au watu binafsi wa habari kwa malipo , kuliko kutegemea wafanyakazi wa
ndani ambao wanaweza kuwa na shuguli nyingine au hawana uwezo mkubwa .

On Aug 18, 6:48 pm, lucs yo <luc...@gmail.com> wrote:
> Wanabidii,
> Tafadhali nihabarisheni, ni nani haswaa anapaswa ku-update hii website ya
> Serikali; inatia aibu kuona bado baraza la mawaziri la zamani lina appear
> kwenye hii website
>
> http://www.tanzania.go.tz/government/cabinet.htm

--
Karibu Jukwaa la http://www.mwanabidii.com/
Pata nafasi mpya za Kazi http://www.kazibongo.blogspot.com/
Blogu ya Habari na Picha http://www.patahabari.blogspot.com/

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.




0 comments:

Post a Comment