Friday 24 August 2012

Re: [wanabidii] Re: KIKWETE AMKATA MAINI MOBHARE MATINYI PIA

                                              WHO IS WHO????
ABDALAH HAMIS OR MOBHARE MATINYI?

Katika mvutano wa maneno huko kwenye ukumbi wa Wanabidii yule anaeitakia vita nyengine Tanzania juu ya ugomvi na Malawi 
(kwasababu alikuwa nje masomoni siku za vita na Nduli Iddi Amin) Bw. Mobhare Matinyi amejibu mapigo aliyoyapata yeye binafsi 
na wenziwe kutoka kwa Rais Kikwete ambae haioni vita kuwa inaweza kuleta manufaa yoyote katika jambo lolote lile katika dunia ya leo. 
Bw. Matinyi akikanusha kule ukumbini kwa Wanabidii kuwa hana jina la uandishi wala la utani, bali .......


N.B.
Jamani mimi ni mjumbe tu. Nimeisoma hii habari huko kwenye blog na 
kwahivyo nisijekuuliwa, kwani mjumbe tunakubaliana kuwa hauwawi!!



From: Abdalah Hamis <hamisznz@gmail.com>
To: wanabidii@googlegroups.com
Sent: Friday, August 24, 2012 7:53:08 AM
Subject: Re: [wanabidii] Re: KIKWETE AMKATA MAINI MOBHARE MATINYI PIA

MAJIBU YA NDUGU  Mobhare Matinyi

Kwanza, jina la safu si jina la mwandishi. Mimi ni Mobhare Matinyi na safu 
inaitwa kwa kutumia jina la ndege tai ambaye sifa yake ni kuwa na macho 
makali. Hii ni kawaida ya majina ya safu. Safu yangu huitwa With an Eagle's 
Eye, na hakuna uthibitisho kwa msomaji yeyote kwamba ni mimi niliyekuja na 
jina hili. Mimi sina jina la uandishi wala la utani, bali hutumia jina 
langu kamili. 
Pili, nilichokieleza kinapaswa kuangaliwa katika muktadha wake, kwamba, 
iwapo Tanzania itanyimwa haki yake, na kuthibitika kwa njia zote kwamba 
imeporwa sehemu ya ziwa, basi italazimika kupigana na hili ni jambo 
linaloungwa mkono na sheria za kimataifa. Ukipigana vita ni lazima umalize 
kazi kwa kuung'oa madarakani utawala ulioileta vita hiyo - - tangu enzi na 
enzi ndivyo ilivyo. Kutoa tamko la maana hii haina maana kwamba mtoa tamko 
anataka vita sasa bali anaikubali vita kama njia ya lazima lakini ya mwisho. 
Tatu, suala la Zanzibar halifanani na la Malawi isipokuwa kwa mtu asiyejua 
anajadili nini. Lakini pia sikusema kitu kuhusu Zanzibar ama Muungano. 
Nne, alichokisema Rais Kikwete hakiondoi uwezekano wa Tanzania kuingia 
vitani. Amesema: "Tuiachie diplomasia ifanye kazi." Kwa mtu mwenye ufahamu 
maana yake ni kwamba Tanzania inataka utatuzi kupitia njia za kidiplomasia 
na lazima uwe kwa manufaa yake. Iwapo Malawi itakataa katu kata, unafikiri 
Kikwete atasema basi tumeshindwa? Hapana! Itafuata njia nyingine kama ya 
kusaka msuluhishi na baadaye mahakama ya kimataifa iitwayo ICJ. Baada ya 
hapo je? 
MUHIMU: Siasa za kimataifa zinahitaji uelewa mpana wa mambo na si 
suala la yeyote kutoa wazo lolote. Haya si masuala ya kila mtu kujisema tu, 
kama ndugu yangu ambaye ameshindwa kuelewa nilichosema na pia ameshindwa 
kupata ulinganifu sahihi. Inahitaji kupekua makarabrasha kwanza ili 
kufahamu matamko ya marais wakati wa hali kama hivi huwa yakoje, sababu za 
nchi kuingia vitani, migogoro ya mipaka ilivyo, sheria za kimataifa, na 
sera ya Tanzania na hata historia pia, achilia mbali siasa. 
Asante, 
Mobhare Matinyi. 

2012/8/24 john mahaba <mahabajo@yahoo.com>
Tusidanganyane hii nchi si mali ya Kikwete kama ingekuwa mali yake asingezunguka nchi
nzima kutuomba ridhaa yetu ili aiongoze, hivyo basi maamuzi yetu ndo kitu cha busara na cha mwisho
na kwa wale wanaofikiri hili limekwisha wanajidanganya tu kwani
msimamo wa Rais WA Malawi ndo unatoa jibu hilo kwani bado yeye anajisimamia
na kuamini wao (WAMALAWI) ndo wenye haki na hilo. na hakuna sehemu yoyote ya katiba ya nchi hii inayompa madalaka
na mamalaka Rais KUUZA, KUGAWA kipande cha nchi hii kwa ridhaa yake mwenyewe.

TUSILETE USHABIKI NA MZAHA KWENYE MASUALA YANAYOHITAJI KUTAFAKARI KWA KINA.


From: alex manonga <manonga2003@yahoo.com>
To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
Sent: Friday, August 24, 2012 9:54 AM
Subject: Re: [wanabidii] Re: KIKWETE AMKATA MAINI MOBHARE MATINYI PIA

Matinyi kama raia wa Tanzania alitoa mawazo yake. Mawazo ambayo kimsingi ni mawazo ya watanzania wengi hasa waishio kando ya ziwa nyasa ambao walitiwa hofu kubwa na uchokozi wa miaka nenda rudi wa majirani zao. Kwa mantiki hiyo wakina Matinyi wako wengi sana lakini bahati mbaya kutokana na kutokuwa na fursa na jukwaa la kutolea mawazo yao ambayo huenda yangekuwa makali zaidi hatukuweza kusoma wala kusikia maoni yao. Huko Mbeya wapo baadhi ya vijana walitamani  serikali iwape silaha ili kulinda nchi. Kwa bahati nzuri katiba yetu ya sasa imeweka marufuku kwa mtu yeyote kumzuia mtanzania kupigania nchi yake. Kumshambulia matinyi binafsi kwa sababu unamuona au una picha yake ni kukosa hoja. Tatizo letu ni mara nyingi kushindwa kutofautisha kati ya mawazo ya mtu na mtu mwenyewe na hutumbukia katika kushambulia mtu badala ya kukosoa mawazo yake. With regard to this 50 years old border dispute, I sometimes agree with Ronald Regan's statement " why should we be innocent in the world that is not innocent?". What kind of a response would we expect could come from a patriot in response to arrogant and impolite statements from the other side of the lake? Sovereignty is always defended- give them an inch and they'll want a mile. Huu ndio ni ukweli na ukweli utabaki ukweli hata kama utapuuzwa na sehemu kubwa ya jamii. 

Alex.


From: Yona F Maro <oldmoshi@gmail.com>
To: Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
Sent: Friday, August 24, 2012 9:02 AM
Subject: [wanabidii] Re: KIKWETE AMKATA MAINI MOBHARE MATINYI PIA

Ndugu ezekiel hili lisikushangaze hapa kwenye mtandao huyu alichofanya
sio cha kwanza na sio wa kwanza kuna wengi wanaoshindwa hoja na kuanza
kutumia lugha chafu au kuleta vitu ambavyo havihusiani na mada husika
ili kukutisha au kukudhalilisha , wengine tunawasamehe na tunaendelea
na maisha kwenye mada nyingine na nyingine katka kupeana elimu na
maarifa lakini ole wao , sio wote wenye moyo wa kusamehe na kusahau na
kuendelea na mengine wengine wanatafutana . Tuwe makini.

On Aug 24, 8:36 am, ezekiel kunyaranyara <ekunyarany...@yahoo.co.uk>
wrote:
> Tony
> Hali hii imetengenezwa, kwa bahati mbaya aliyeitengeneza hakujua yanayoweza kutokea. Haya sasa ndiyo matokeo yake. Kwa nionavyo mimi bado yatatokea makubwa zaidi. Kuna haja kuja kama taifa kufungua macho katika hali kama hii ya kutopendana. matinyi ni Mzalendo hasa, na kwa mchango wake hapa jukwaani kasaidia sana kulinenepesha kwa hoja zake nzuri na za uchambuzi. Mtizamo wake katika hoja ya Malawi ni mtizamo wa watu wengi nikiwemo na mimi. Lakini kutofautiana mtizamo na JK siyo tatizo kwani naye hadi kufikia hapo kapata ushauri wa kila aina. Na nivizuri kama watanzania kujua kwamba pamoja na kauli ya Mkuu wa nchi lakini lazima kuchukua tahadhali sana na Malawi ni watata.
>
> K.E.M.S.
>
> ________________________________
>  From: Tony PT <tony_u...@yahoo.co.uk>
> To: wanabidii@googlegroups.com
> Sent: Thursday, 23 August 2012, 0:19
> Subject: Re: [wanabidii] KIKWETE AMKATA MAINI  MOBHARE MATINYI PIA
>
> Elisa,
>
> Nchi hii imefikiia pabaya sana na kuna siku sisi wenyewe tutatwangana tu humu na wala sio Malawi!
>
> Angalia kichwa cha habari ni very Sadistic na kwa siku mbili naona watu wakimbeza Matinyi, Kafumu n.k. Yote hii ni chuki binafsi juu ya watu; mtu na akili zake anafurahia mtu mwingine kuharibikiwa au kupotelewa na alichokuwa nacho...hii ni sifa kamili ya unyama, kutopendana na kutohurumiana!
>
> Sijui nani ataisahihisha hali hii maana inazidi kwa jamii yetu na hasa rika la kati ya miaka 20-35! Tukienda na mwendo huu wa kiinyama, hatufiki mbali tutapigana tu! Sio ustaarabu kuchukiana kwa kitu ambacho kinamhusu mtu au binadamu mwenzako. Sijui siasa ndiyo inatuelekeza huku au ukosefu wa maadili mema tu. Inasikitisha sana!
> Sent from my BlackBerry® Porsche-9981 smartphone Thru Tigo Network, Tanzania.
> ________________________________
>
> From:  ELISA MUHINGO <elisamuhi...@yahoo.com>
> Sender:  wanabidii@googlegroups.com
> Date: Wed, 22 Aug 2012 03:57:35 -0700 (PDT)
> To: <wanabidii@googlegroups.com>
> ReplyTo:  wanabidii@googlegroups.com
> Subject: Re: [wanabidii] KIKWETE AMKATA MAINI  MOBHARE MATINYI PIA
>
> Kichwa cha habari na maelezo haya yangesubiri mgogoro wa mpaka ukaisha ndipo yaandikwe. Majeshi si ya Kikwete ni ya kulinda nchi. Kikwete akiamua kuiuza nchi yatailinda. Ili mradi mazungumzo yanaendelea na Malawi 'have not listened' Huwezi kuiondoa Military option eti kwa kuwa Rais kasema. Anaweza kulazimika kubadili usemi wake. Hatujasikia rais akizuia watanzania kutochota maji ya ziwa Nyasa kwa kuwa ameamua ni mali ya Malawi. Hatujasikia wavuvi wa Tanzania wameenda kuvua wakatekwa na Rais akasema shauri lao. Yakichagiza hayo atasema anafuta kauli.
> Omba mazungumzo yafanikiwe la sivyo anaweza kulazimika/kulazimishwa kubadili kauli
> Au siyo!
>
> --- On Tue, 8/21/12, John Nkumbaruko <nkumbar...@yahoo.com> wrote:
>
>
>
>
>
>
>
>
>
> >From: John Nkumbaruko <nkumbar...@yahoo.com>
> >Subject: [wanabidii] KIKWETE AMKATA MAINI MOBHARE MATINYI PIA
> >To: "wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com>
> >Date: Tuesday, August 21, 2012, 5:32 PM
>
> >KIKWETE AMKATA MAINI
> >MOBHARE MATINYI PIA!
>
> >•Bw. Matinyi kazizowea siasa za kikoloni
> >•Hata Unguja atataka ivamiwe ikitaka kuacha Muungano
>
> >Zanzibar, Tanzania
> >Kwa RAIS Jakaya Kikwete kusema kuwa hajaliagiza Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kupigana vita na Malawi kwa sababu za mpaka wa Ziwa Nyasa
> >kati ya nchi hizo mbili aliwakata maini sio Membe na Lowassa tu, bali mpaka yule muandishi mkorofi wa gazeti la The Citizen anaejulikana kwa jina la
> >mapambano (nom de guerre) kama Mr Eagle, wakati jina lake hasa ni Mobhare Matinyi.
> >Katika ukumbi wa Wanabidii Bw. Matinyi bila ya haya na bila ya kuwa amelewa gongo alinukuliwa akiandika…" …invade Malawi (because Lilongwe won't listen),
> >kick out every stupid guy and restore a new sensible government. We did it in Uganda, why not in Malawi? After all Joyce Banda has already said that she
> >is ready to die for her country - so let us help her."
>
> >Read more »www.zanzibarnikwetu.blogspot.co.uk
>
> >--
> >Karibu Jukwaa lawww.mwanabidii.com
> >Pata nafasi mpya za Kaziwww.kazibongo.blogspot.com
> >Blogu ya Habari na Pichawww.patahabari.blogspot.com
> >
> >Kujiondoa Tuma Email kwenda
> >wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
> >
> >Disclaimer:
> >Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
> >
> >
>
> --
> Karibu Jukwaa lawww.mwanabidii.com
> Pata nafasi mpya za Kaziwww.kazibongo.blogspot.com
> Blogu ya Habari na Pichawww.patahabari.blogspot.com
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
>
> Disclaimer:
> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
>
>
>
> --
> Karibu Jukwaa lawww.mwanabidii.com
> Pata nafasi mpya za Kaziwww.kazibongo.blogspot.com
> Blogu ya Habari na Pichawww.patahabari.blogspot.com
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
>
> Disclaimer:
> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.




--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 


--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 


0 comments:

Post a Comment